ZABURI 127:3-5

Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu. Kama mishale mkononi mwa shujaa, Ndivyo walivyo wana wa ujanani.

MATHAYO 18:4

Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.

MITHALI 22:6

Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.

KUMBUKUMBU LA TORATI 11:19

Nayo wafunzeni vijana vyenu kwa kuyazungumza uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo

MATHAYO 18:10

Angalieni msidharau mmojawapo wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni.

Wednesday, February 10, 2016

WATOTO NI MALI YA BWANA

Marko 10:14 Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.

MALEZI KWA WATOTO NI JAMBO LA MSINGI SANA

Mithali 22 : 6

 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.